Katika mahojiano na gazeti la Kommersant Jumatatu, Lavrov alisema utandawazi wa uchumi wa dunia umeharibiwa baada ya vikwazo kuwa "chombo pekee cha sera ya nje ya [rais wa zamani wa Marekani, Joe Biden]."
Mwanadiplomasia huyo mkuu wa Russia amebainisha kuwa, utawala wa Rais Donald Trump umeanza kujadili ushirikiano wa kibiashara na kiuchumi na Moscow.
Kwa mujibu wa Lavrov, ushirikiano wa kiuchumi kati ya nchi hizo mbili umeshuka "kwa takriban 95% ikilinganishwa na kilele cha karibu dola bilioni 30 miaka kumi iliyopita, haswa kutokana na vikwazo visivyo halali."
Ushirikiano wa siku zijazo utategemea kabisa Washington, Lavrov amesema akisisitiza kwamba, "Hatumfukuzi mtu yeyote au kuomba vikwazo viondolewe."
Washington na washirika wake waliweka vikwazo vikali dhidi ya Moscow baada ya Crimea kuungana tena na Russia mnamo 2014, na baadaye kuongeza vingine kwa madai ya Moscow kuingilia uchaguzi wa Marekani.
Vikwazo hivyo vilipanuliwa kwa kiasi kikubwa na utawala wa rais wa zamani wa Marekani Joe Biden kufuatia kuongezeka kwa mzozo wa Ukraine mwaka 2022.
342/
Your Comment